Jumapili 5 Julai 2026 - 08:53
“Labbaik Sayyid Mujtaba”; Kaulimbiu ya Wananchi katika Hafla Kuu ya Kumuaga Kiongozi Shahidi wa Iran

Hawza/ Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kwa kutegemea misingi halisi ya dini na kuasisi mfumo wa Wilayat al-Faqih, imejenga mkakati wake wa kuunda utambulisho wa taifa juu ya msingi wa uhusiano usiovunjika kati ya uongozi na wananchi; uhusiano ambao umeendelea kuwa mwiba machoni mwa maadui wa ubinadamu, dhamana ya kudumu kwa malengo ya Mapinduzi ya Kiislamu, na taa ya matumaini kwa wapigania haki na waliodhulumiwa katika pembe zote za dunia.

Mfumo wa kisiasa wa Iran umejengwa juu ya nguzo imara ya Wilayat al-Faqih; mfumo ambao si tu mfano wa uongozi wa dola, bali pia ni dhihirisho la uhusiano wa moyoni na wa kiitikadi kati ya Umma na Kiongozi. Nafasi hii ni zaidi ya mfumo wa kawaida wa kiutawala; ni ngome ya uthabiti wa nchi mbele ya dhoruba kali za kisiasa na vitisho vya kutoka nje. Azma na mshikamano wa wananchi na mhimili huu wa uongozi wa Kiwilaya ni ukweli ambao hakuna shinikizo, vikwazo wala njama zilizoweza kuuvunja; kwa sababu mshikamano huu una mizizi katika imani ya msingi wa dini ambayo imefungamana kwa kina na roho pamoja na utambulisho wa Wairani, na hivyo kuendeleza upya azma ya kitaifa ya kulinda uhuru na heshima ya nchi.

Kwa muda wote ambao utiifu huu wa kujitambua na imani hii thabiti vinaendelea kuishi ndani ya jamii, matumaini ya kupatikana kwa uadilifu na uhuru nchini Iran pamoja na miongoni mwa wanyonge na waliodhulumiwa wote duniani yataendelea kubaki hai. Ustahimilivu huu, kwa hakika, umeunda kizuizi kisichopenyeka dhidi ya tamaa za kujitanua za kambi ya ubeberu na maadui wa ubinadamu. Katika mantiki ya muqawama, imani hii pamoja na matumaini ya pamoja ndivyo ambavyo vimekuwa kama mwiba machoni mwa wenye nia ovu, na mara kwa mara vimeharibu hesabu zao za kutaka kuyapigia magoti mataifa huru. Huu ni ukweli ambao umeifanya Iran kuwa kitovu cha kutoa hamasa kwa harakati zote za kudai haki katika pembe zote za dunia.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha